Daud Mwangosi ameuwawa jana katika vurugu za Polisi na wafuasi wa CHADEMA katika kijiji cha Nyololo, Mufindi, Iringa.
Mwangosi aliuwawa majira ya saa 10 jioni katika ofisi za CHADEMA Nyololo huku askari mmoja akijeruhiwa vibaya kwa risasi.
Kabla
ya kuuawa kwa mwanahabari huyo, mabomu yalipigwa eneo hilo ili
kuwatawanya wafuasi wa CHADEMA ambao walikuwa wakigoma kutawanyika eneo
hilo na kuamua kukaa chini kuwa hawapo tayari kuondoka katika ofisi yao.
Chanzo
cha mwanahabari Mwangosi kuuwawa kilitokana na kukamatwa kwa mwandishi
wa habari wa gazeti la Nipashe mkoa wa Iringa, Godfrey Mushi na hivyo
mwanahabari huyo kutaka kuhoji polisi sababu ya kukamatwa kwa
mwanahabari huyo ndipo askari hao walipoanza kumshambulia kwa kichapo na
baadaye mlio kama wa bomu ulisikika eneo hilo na mwandishi huyo na
askari mmoja waliaguka chini.
Ndani ya dakika tano ilisikika
sauti kutoka kwa askari huyo kuwa afande nimekufa ndipo walipomchukua na
kumpeleka Hospitali ya wilaya ya Mufindi huku mwili wa mwanahabari huyo
ukipelekwa chumba cha kuhifadhia maiti.
Katika vurugu hizo
zilizodumu kwa takribani dakika 30 kwa askari na wafuasi wa CHADEMA
kurushiana mawe kwa mabomu, zaidi ya magari matano ya CHADEMA na ya
wananchi yameharibiwa, huku watu kadhaa wakiachwa wamejeruhiwa hali
mwanahabari mmoja, Godfrey Mushi akijeruhiwa vibaya. Source: http://francisgodwin.blogspot.com/ |
No comments:
Post a Comment